Tuesday, November 28, 2017

Audio | Diamond Platnumz – Niache | Mp3 Download

Audio | Diamond Platnumz – Niache | Mp3 Download

Diamond Platnumz - Niache

Audio | Diamond Platnumz – Niache | Mp3 Download


                                         DOWNLOAD HERE

Sunday, November 26, 2017

NOMA!!! MR. Blue ''KASEMA KAMA SIO FIESTA???

NOMA!!! MR. Blue ''KASEMA KAMA SIO FIESTA???




MR. Blue alivyompandisha Nyandu Tozi kwenye Stage ya Fiesta DSM

MR. Blue alivyompandisha Nyandu Tozi kwenye Stage ya Fiesta DSM



YA MOTO BAND: Wamerudi tena ni kwenye stage ya Fiesta DSM kwa Pamoja


BALAA LA WOWOWO !!! Zaiid kafunika FIESTA DSM !!!! + OMG

BALAA LA WOWOWO !!! Zaiid kafunika FIESTA DSM !!!! + OMG




UJANJA WA DOGO JANJA FIESTA DSM !! TipTop hawajakosea

UJANJA WA DOGO JANJA FIESTA DSM !! TipTop hawajakosea



Mume wa Irene Uwoya kazini ! kazi ya Dogo Janja FIESTA DSM

Mume wa Irene Uwoya kazini ! kazi ya Dogo Janja FIESTA DSM



Moto wa Country Boy na Baraka The Prince FIESTA DSM


MABIBI NA MABWANA !! Hii ndio ya Alikiba FIESTA DSM

MABIBI NA MABWANA !! Hii ndio ya Alikiba FIESTA DSM



FIESTA DSM... Moto wa Rosa Ree na Chin Beez

FIESTA DSM... Moto wa Rosa Ree na Chin Beez



HAWA HAPA !! Mimi Mars na Lulu Diva FIESTA DSM

HAWA HAPA !! Mimi Mars na Lulu Diva FIESTA DSM



NI ROSTAM TENA!! NANI MKALI??? FIESTA DSM HIYO..

NI ROSTAM TENA!! NANI MKALI??? FIESTA DSM HIYO..




Pambano la Kimataifa la Mwaka Kati ya Ibrahim Class na Koos Sibiya

Pambano la Kimataifa la Mwaka Kati ya Ibrahim Class na Koos Sibiya


Maagizo ya simu aliyopiga Rais Magufuli kwenye FIESTA leo Alfajiri

Maagizo ya simu aliyopiga Rais Magufuli kwenye FIESTA leo Alfajiri



Mziki wa G, Nikk na Joh... Mtu 3 FIESTA DSM




Mziki wa G, Nikk na Joh... Mtu 3 FIESTA DSM




"JUX KANIWEZA" - VANESSA MDEE




"JUX KANIWEZA" - VANESSA MDEE



"Bado siamini, nisingependa iwe hivyo kwa Vanessa" - JUX


Nguvu ya Aslay FIESTA Dar es salaam


Moto wa Rich Mavoko FIESTA DSM

Moto wa Rich Mavoko FIESTA DSM


Hapa Ommy Dimpoz Huku Christian Bella ''NANI KAMA MAMA''

Hapa Ommy Dimpoz Huku Christian Bella ''NANI KAMA MAMA''



Mahaba mazito ya Jux.. kam-kiss Vanessa FIESTA

Mahaba mazito ya Jux.. kam-kiss Vanessa FIESTA


Tuesday, November 21, 2017

MAGAZETI YA LEO 22/11/2017

MAGAZETI YA LEO 22/11/2017





















KWA MIAKA 16: Hiki ndicho Kikosi Bora cha UEFA Champions League


KUTOKA AFRIKA : Mastaa wa Kike wanaokimbiza Hollywood


BREAKING NEWS: Ajali ya moto iliyotokea ofisi za Clouds Media


Zelothe azungumza kimasai wakati akiomba kura



  Arumeru. Vituko na vioja vimezidi kutawala kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani Kata ya Musa mkoani hapa baada ya mgombea udiwani kupitia CCM, Flora Zelothe kuamua kuongea kimasai kwa lengo la kuwashawishi wananchi wampe kura.

Zelothe, aliamua kutumia lugha hiyo juzi wilayani Arumeru kama njia mojawapo ya kuwashawishi wapigakura wa eneo hilo ambao kwa asilimia kubwa ni makabila ya Wameru na Wamasai.

Akizungumza katika mkutano huo, Zelothe alisema wananchi wakimchagua atatekeleza mradi wa maji uliokuwa unagharamiwa na Benki ya Dunia eneo la Makutian ambao umesimama baada ya kuvurugwa na baadhi ya wanasiasa.

Akinadi sera zake kwa kimasai huku akiwa na mtafsiri wake pembeni aliwaambia wapigakura amejipanga kujenga shule ya sekondari.

Alisema kwa miaka mitano akiwa diwani wa viti maalumu alifanikiwa kuchonga barabara zote za vitongoji ndani ya Kata ya Musa kwa kiwango cha changarawe.

“Tutaboresha Shule ya Sekondari ya Kata ya Musa na kuleta walimu wa masomo ya sayansi na sanaa,” alisema Zelothe huku akishangiliwa.

Awali akimkaribisha jukwaani mwenyekiti wa CCM mkoani Arusha, Lekule Laiser alisema mgombea huyo ni mwanamke lakini ni jasiri na anajenga hoja.

Laiser alisema Zelothe aliwahi kwenda kupinga matokeo ya uchaguzi wa udiwani wa kata hiyo mwaka 2015 mahakamani na kusimamia kesi bila kuyumba na hilo linaonyesha dhahiri anafaa kuwa kiongozi. 


Nafasi za kazi leo November 21

BoT imeeleza hali ya uchumi wa Tanzania kwa miaka 10 iliyopita

BoT imeeleza hali ya uchumi wa Tanzania kwa miaka 10 iliyopita


Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imeeleza  kuwa, Tanzania ni miongoni mwa nchi za Afrika zenye uchumi unaokua kwa kasi barani Afrika katika kipindi cha muongo mmoja uliopita yaani kuanzia mwaka 2007  hadi  2016
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchumi BoT, Johnson Nyella jana jumatatu kwenye sherehe ya Siku ya Takwimu Afrika (2017), iliyofanyika kitaifa jijini Dar es Salaam ambapo alieleza kuwa  uchumi wa Tanzania ulikua kwa wastani wa asilimia 6.7 mwaka 2016, wakati pato la taifa lilikua kwa wastani wa asilimia 7, sawa na ilivyokuwa mwaka 2015 na 2014.

Bw. Nyella amesema  kwa miaka minne mfululizo, mfumuko wa bei wa Taifa umeendelea kupungua na kubaki katika kiwango cha tarakimu moja.

“Mwaka 2016 mfumuko wa bei ulipungua na kufikia wastani wa asilimia 5.2 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 5.6 mwaka 2015 na asilimia 6.1 mwaka 2014.” amesema Nyella huku akielezea umuhimu wa Takwimu bora.

Takwimu bora za uchumi zinahitajika katika kupanga mipango ya maendeleo na utungaji wa sera kwa ajili ya kuboreshamaendeleo endelevu ya mwaka 2030.

Kwa mujibu wa Nyella, takwimu bora za kiuchumi zinasaidia kuongeza tija serikalini katika kupanga mipango ya maendeleo na kukabiliana na changamoto kadri zinavyojitokeza.

Amesema takwimu bora pia zinawasaidia watunga sera na watekelezaji wa programu mbalimbali na kupanga mikakati mipya ya kuboresha maisha ya wananchi.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), Dkt. Albina Chuwa amesema kwenye sherehe hizo kuwa, takwimu bora za uchumi ni muhimu katika kufikia ajenda ya Bara la Afrika ya mwaka 2063 inayosisitiza ukuaji wa uchumi.

Katika kufikia ajenda hiyo, baadhi ya mambo yanayosisitizwa ni amani, utulivu, kuboresha uchumi wa Afrika, kukusanya mapato ya Afrika ili Afrika iweze kujitegemea.

Dk Chuwa, amesema Kamisheni ya Umoja wa Mataifa ya Uchumi ya Afrika (UNECA) kwa kushirikiana na Ofisi za Takwimu za Afrika, ina kaulimbiu isemayo “Takwimu Bora za Uchumi kwa Maisha Bora” ikisisitiza umuhimu wa takwimu za kiuchumi katika kuleta maendeleo endelevu hivyo kuboresha maisha ya wananchi.

Kaulimbiu hiyo inaakisi juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano ya Rais John Magufuli kwa kuwa na dhamira ya kutengeneza uchumi wa viwanda. Amesema kwa sababu hiyo, takwimu rasmi za uchumi za serikali lazima zitolewe kwa weledi na kwa kufuata kanuni na sheria.

“Takwimu bora za uchumi kwa nchi yetu ni za muhimu sana, hasa wakati huu ambao Serikali yetu inaimarisha uchumi wa viwanda ili Tanzania iweze kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025 na kuboresha zaidi maisha ya wananchi. Takwimu hizi za uchumi ni pamoja na takwimu za kilimo, viwanda, ujenzi, usafirishaji, nishati, biashara, mazingira, mfumuko wa bei na uwekezaji.”amesema Dkt. Chuwa.

Dkt. Chuwa amesema takwimu bora ni takwimu zilizo sahihi, zinazotolewa kwa wakati, linganifu na za kina, zinazozalishwa mara kwa mara na zenye ufanisi. Dk Chuwa alisema, sifa hizo zote zinaendana na kanuni za msingi za takwimu rasmi za Umoja wa Mataifa na Mkataba wa Takwimu wa Afrika, ambazo maisha ya wananchi, hasa kutekeleza ajenda.

Real Madrid yamuacha Ramos

Nahoda wa Real Madrid Sergio Ramos ameachwa kwenye kikosi kilichosafiri kwenda nchini Cyprus kucheza na Apoel Nicosia leo kwenye mchezo wa hatua ya makundi ya ligi ya mabingwa Ulaya.

Sergio Ramos alivunjika pua kwenye mchezo wa La Liga jumamosi iliyopita wakati timu yake ya Real Madrid ilipotoka sare ya bila kufunagana na Atletico Madrid kwenye uwanja wa Wanda Metropolitano.
Mlinzi huyo wa kati mwenye miaka 31, bado haijajulikana atarejea lini uwanjani. Ramos anaongeza idadi ya majeruhi kwenye timu hiyo akiwemo winga Gareth Bale pamoja na golikipa Keylor Navas.

Mabingwa hao watetezi wa UEFA wameshinda mechi moja tu katika michezo yao minne iliyopita kwenye mashindano yote.

Katika kundi H Real Madrid ina nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya 16 bora pamoja na timu ya Tottenham Hotspurs ambayo itakuwa ugenini leo nchini Ujerumani kukipiga na wenyeji Borussia Dortmund

Nasa kuzuiwa kuanzisha Mabaraza ya Wananchi




Nairobi, Kenya. Mahakama Kuu imetoa amri ya kuzuia mabaraza yote ya kaunti kupitisha au kutekeleza hoja ya kuanzishwa mabaraza ya wananchi, jambo ambalo linatajwa kuwa pigo kwa muungano wa upinzani (Nasa).

Jaji Lilian Mutende alitoa amri ya muda Jumatatu hadi ilitakapokamilika kusikilizwa kesi iliyofunguliwa na wanaharakati Counties Development Group.

"Amri hii inatolewa kuwazuia walalamikiwa kuanzia wa nne hadi 50 na wanachama na wajumbe wa mabaraza ya kaunti kutoanzisha mchakato wa kuteua wajumbe, timu na waangalizi wa Baraza la Watu,” inasema amri.

Kesi iliyofunguliwa Jumatatu mchana ikiomba kuwazuia wawakilishi kutoatekeleza hoja iliyowasilishwa na kufikishwa mbele yao kwa ajili ya kuteua au kuchagua wanachama au wajumbe au waangalizi wa mabaraza ya wananchi.

Amri ya Jeji Mutende itadumua hadi Januari 28 mwaka ujao wakati usikilizwa wa kesi ukiendelea. Hata hivyo, mkuu wa sekretarieti ya Nasa walioanzisha utaratibu wa kuunda mabaraza ya wananchi, Norman Magaya alitupilia mbali amri hiyo akisema “upuuzi".

Sophia Simba arudi CCM



Dar es Salaam. Aliyekuwa Mwenyekiti wa Wanawake CCM (UWT), Sophia Simba aomba radhi na kuomba kurejea CCM baada ya kufukuzwa uanachama.

Mwenyekiti wa CCM Rais John Magufuli amesoma barua ya Sophia kuomba radhi mbele ya Kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC) na kuwahoji wajumbe kama wanakubali kumsamehe jambo lililokubaliwa.

"MwanaCCM aliyefukuzwa uanachama amekuwa akiandika barua nyingi za kuomba radhi lakini tumekuwa tukinyamaza,  kikao hiki ndiyo kilimfukuza," amesema Rais Magufuli katika kikao hicho kinachofanyika leo Jumanne.

Baada ya kuwahoji wajumbe na kukubaliwa Rais Magufuli aliandika kwenye barua hiyo kuwa amekubaliwa kurudi CCM.

Ruge kukutana na Makonda Kuhusu Tamasha la Fiesta



Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba, Jumatatu hii amefunguka kuzungumzia tetezi ya kwamba Tamasha la Muziki la Fiesta litaishia 6 usiku tofauti na miaka iliyopita kutokana na hali ya usalama.

Hatua hiyo imekuja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda hivi karibuni akiwa katika kituo cha redio cha EFM kuzungumza juu ya matukio ya burudani kutotakiwa kufanyika zaidi ya saa sita usiku kwenye maeneo ya wazi Dar es salaam.

Tamasha la FIESTA 2017 linatarajiwa kufanyika Leaders Club Jumamosi hii November 25 huku ticket tayari zikiwa zimeshazagaa mitaani.

Ruge ambaye ni Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalishaji Clouds Media Group amesema “Tunafanya juhudi za kujaribu kuona kama tunaweza tukampata Mkuu wa Mkoa”

Profesa Kitila, Katambi, Msando waingia CCM



Dar es salaam. Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji, Profesa Kitila Mkumbo ametangazwa rasmi leo Jumanne mbele ya mkutano wa NEC, CCM unaoendelea Ikulu jijini Dar es salaam.

Mbali na Profesa Kitila ambaye alikuwa kada wa ACT, pia kuna Mwenyekiti wa Bavicha, Patrobas Kitambi ambaye ni Mwenyekiti wa Bavicha, Lawrence Masha, Samson Mwigamba na Albert Msando.

Akizungumza mbele ya mkutano huo, Profesa Kitila amesema: "Nguvu ya CCM zipo tano, moja ni kwamba ni chama cha watu, ni chama pekee chenye nguvu siyo chama kuogopa watu, tulijaribu huko tulipokuwa lakini yalishindwa."

Kwa upande wake, Masha amesema alipoamua kuondoka, baba yake alisikitishwa na uamuzi huo lakini baada ya kutafakari ameamua kurejea nyumbani.

Amesema yeye ni mwanaCCM na kijana alilelewa ndani ya chama hicho.

"Mwenyekiti wewe ni mfugaji, ng'ombe akiingia zizini amekatwa mkia unamwangalia mara mbili mbili, mimi sijakatwa mkia ni mwaminifu, ukinihitaji nitumie, kudumu Chama cha Mapinduzi," amesema Masha.

Kwa upande wake Mwigamba amesema hoja zote walizopigania Rais John Magufuli kwa sasa anazitekeleza. Kutokana na hali hiyo analazimika kumuunga mkono.

"Lakini ni bahati mbaya wapo wanaoamini upinzani ni kama, tumeamua kuwa moto, wanaposema huyo amenunuliwa, mie ndiyo naendelea kuwa moto.”

Yeye Msando amesema  baada ya kutoka Chadema kwenda ACT amejitambulisha rasmi kujiunga na chama hicho.

Amesema anafarijika kuona chama hicho na haoni aibu kuwa karibu na CCM tofauti na ilivyokuwa miaka ya zamani kwani wanachama walihofia kuvaa mavazi ya chama hadharani kwa kuogopa kuzomewa.

"Kwa sasa chini ya uongozi wako, mtu anajivunia kuwa mwanachama wa CCM, tukaona juhudi zinazoendelea," amesema Msando.

Mourinho aandaa mpango mpya Man United



Hakuna bata! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya kocha wa Manchester United, Jose Mourinho kukipangia kikosi chake programu ya kufanya mazoezi Siku ya Krismas kwenye Uwanja wa Old Trafford kutoka uwanja wao wa kawaida wa mazoezi, Carrington.

Mourinho, amewapangia programu hio mpya wachezaji wake kuelekea kwenye mchezo wa Siku ya Kupeana Zawadi (Boxing Day) dhidi ya Burnley itakayoanza saa 11 jionii  ndani ya dimba hilo.

Maamuzi hayo ya kuhama Carrington, ndani ya Krismas yanatarajia kuwahusisha wafanyakazi wengine 50 au zaidi ambao watakua kwenye majukumu mbali mbali siku hio huku wakikosa kuutumia muda huo kujivinjari na familia zao.

Mazoezi ndani ya viwanja vya Carrington hujumuisha wafanyakazi 20 lakini kufuatia mabadiliko hayo, idadi ya wafanyakazi inatarajiwa kufikia hadi 70 watakaoshughulikia masuala mbali mbali ikiwemo ulinzi na uandaaji wa dimba hilo.

Nape afunguka kuhamia upinzani

Nape afunguka kuhamia upinzani




Mtwara. Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Nauye amesema hana mpango wa kuhama CCM kwenda upinzani na badala yake ametaka vyama hivyo visipoteze muda kudhania atahama.

Nape ametoa kauli hiyo jana Jumatatu jioni wakani wa kampeni za kumnadi mgombea udiwani wa Kata ya Reli, Genfrid Mbunda katika uwanja wa Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Alisema wapinzani wasipoteze muda wakimsubiri kuwa atahama CCM kutokana kwamba CCM ni chama bora kuliko vyama vyote vya siasa hivyo hawezi kutoka ndani ya chama hicho.

“Unajuwa wapinzani wasipoteze muda wa kusubiri mimi lini nitahama CCM badala yake wafanye kazi ya kuvijenga vyama vyao kwa sababu walitamani sana muziki huu uhamie kwao ndio maana wanabaki wanapiga kelele za kuwapa presha wanaCCM hivyo sitahama kwa sababu ukinikata mwili wangu damu yangu unakuta CCM,” alisema Nape.

Alisema kuwa CCM hakwenda kwa bahati mbaya kutokana kwamba anakijua chama hicho hivyo hakuna namna yoyote itakayoweza kumtenganisha na chama hicho.

“Kupitia changamoto katika mabonde na mawimbi ndio unaandaliwa kuwa mkomavu na kupanda juu kwa sababu ukikimbia mapema unaonekana haufahi lakini ukibaki na kuvulimia milima na mabonde ndio unaokana ni mkomavu na ukizingatia ndani ya chama hiki kuna fursa za kutosha,” alisema.

“Kupitia mabonde na milima bila kuyumba nitaendelea kusimama imara ndio maana nikaaminiwa sasa wanaodhani Nape anapitia milima na mabonde kwa sababu hata mbegu ili iote ni lazima upande chini ili iweze kuota na hiyo ndio fomula ya maisha sasa wakati mbegu inaoza watu wanaanza kuongea siji ng’o,” aliongeza Nape.

“Mimi bado sijaona mawimbi yanayoweza kumkimbiza  CCM bado nimesimama imara kwa ajili ya kupambana na mawimbi hakuna mabadiliko yasiyo na machungu hata mama mjazito hupata machungu lakini hufurahi kupata mtoto baada ya kuvumilia kwa muda mrefu,” alisema Nape.

Watanzania kukutwa na heroini Swaziland



   Dar es Salaam. Watanzania watatu wamekamatwa nchini Swaziland kwa tuhuma za kukutwa na kilogramu 30 za dawa za kulevya aina ya heroini zilizokuwa zinapelekwa Afrika Kusini.

Kamishna mkuu wa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA), Rogers Sianga alisema jana kuwa Watanzania hao walikamatwa mpakani mwa nchi ya Msumbiji na Swaziland wakiwa na mzigo huo.

“Kinachofanyika sasa ni kwamba tunashirikiana na nchi ya Swaziland ili kujua watanzania hao wanashirikiana na akina nani na mtandao wao kwa ujumla,” alisema Sianga.

Taarifa zinadai kuwa Watanzania hao walikamatwa juzi na maofisa wa polisi wa Swaziland wakiwa na dawa za kulevya zilizofichwa ndani ya buti la gari.

Maofisa hao baada ya kufanya upekuzi walibaini mifuko ya plastiki miwili ya rangi nyeusi.

Inadaiwa kuwa kila pakiti yenye dawa hizo iliwekwa pilipili ili kuzuia mbwa waliokuwa wanatumiwa kupekuwa wasibaini harufu za dawa hizo za kulevya.

“Kwa kuwa sasa hivi tumewabana wafanyabiashara hao haramu wa dawa za kulevya, wameamua kukimbilia Msumbiji kwa ajili ya kufanya biashara hiyo. Soko kuu lipo Afrika Kusini na mara nyingi wanawawekea dhamana (bond) vijana kusafirisha na wanapofanikiwa wanalipwa fedha zao,” alisema.

Alifafanua kuwa kutokana na kushamiri kwa wafanyabiashara hao, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya imefanyiwa marekebisho ya sheria mpya kifungu cha 15 ikiwamo kuongezea kosa la kuweka mtu rehani kwa minajili ya kufanikisha biashara hiyo, huku adhabu yake ni kifungo cha maisha jela.

Kamishna wa Kitengo cha Huduma za Sheria, Edwin Kakolaki alisema makosa mengine chini ya kifungo hicho ni kusafirisha dawa za kulevya na kuchepusha, kusafirisha isivyo halali kemikali bashirifu.

Kakolaki aliongeza kwamba marekebisho mengine ya sheria hiyo ni kuipa uwezo mamlaka hiyo kushughulikia makosa mengine yenye uhusiano wa moja kwa moja na biashara na matumizi ya dawa za kulevya kifungu cha 4(2)(f).

Zaidi ya hilo pia alisema kwamba marekebisho mengine yanampa uwezo kamishna jenerali kushikilia akaunti za benki za mtuhumiwa kwa muda, kwa mujibu wa kifungu kipya cha 50A kwa wauzaji wa dawa za kulevya za kiwandani.

“Pia, adhabu kwa makosa hayo itakuwa kifungo miaka 30 bila faini, ikumbukwe kuwa adhabu hii haiwahusu watumiaji wa dawa za kulevya ambao sheria inawachukulia kama wagonjwa endapo kutakuwa na uthibitisho wa daktari kwamba ni watumiaji na wameathirika na dawa hizo,” alisema Kakolaki. 

Breaking News: Clouds Media Group inawaka moto

Sehemu ya jengo la kituo cha Chouds Media Group linaungua moto muda huu. Juhudi za kuuzima moto huo bado zinaendelea.

Monday, November 20, 2017

Bilioni tano zaokolewa

Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Ubongo, Mgongo na Mishipa ya Fahamu (MOI) imeokoa zaidi ya shilingi Bilioni 5 ambazo zingetumika kusafirisha wagonjwa nje ya nchi kufuata matibabu.





Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii , Jinsia Wazee na watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya alipotembelea MOI na kukagua hali ya utoaji wa huduma, mazingira , miundombinu na kuwajulia hali wagonjwa pamoja na kukutana na menejimenti.

Dkt. Mpoki amesema kuwa fedha hizo zimeokolewa baada ya MOI kuanzisha huduma za kibingwa ambazo awali zilikua hazipatikani hapa nchini, hivyo kulazimu wagonjwa kwenda kutibiwa nje ya nchi hivyo kuongeza gharama.

Akizungumza na uongozi wa MOI, Dkt. Ulisubisya amepongeza kazi nzuri na kubwa inayofanywa ambayo imepelekea watanzania kupata huduma bora za kibingwa ambazo wangepaswa kuzifuata nje ya nchi.

Aidha, Dkt Ulisubisya amesema MOI imepunguza rufaa za kwenda nje ya nchi kwa asilimia 95% na asilimia 5% iliyobaki MOI inaweza kuimaliza kabisa na kusiwepo na mgonjwa wa kwenda nje ya nchi.


Audio | Diamond Platnumz – Niache | Mp3 Download

Audio | Diamond Platnumz – Niache | Mp3 Download Audio | Diamond Platnumz – Niache | Mp3 Download                               ...